Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Muheza Mhe. Ayubu Sebabili mapema leo Februari 10, 2026 amerejesha tabasamu la wananchi wa Kijiji cha Muungano kilichopo katika Kata ya Mlingano baada ya Kumpumzisha Mwenyekiti wa Kijiji hicho Mhe. Michael Frank Lupa kufuatia tuhuma mbalimbali zilizotolewa na baadhi ya wananchi wa kijiji hicho dhidi ya kiongozi huyo.
Kauli hiyo ameitoa mbele ya Mkutano Mkuu wa Kijiji uliofanyika katika Kitongoji cha Machema, kijiji cha Muungano kata ya Mlingano'
Mkuu huyo wa Wilaya amesema ameunda Tume ya kuchunguza tuhuma zilizotolewa dhidi ya Mwenyekiti huyo ikiwa ni pamoja na ukataji wa miti ya mivule holela bila kuzingatia kanunni na taratibu za uvunaji wa miti zilizowekwa kwa mujibu wa Sheria sambamba na ubadhilifu wa mali za umma.
Amesema Tume hiyo itafanya kazi ndani ya siku 30 ikibainika kuwa Mwenyekiti ametenda kosa atachukuliwa hatua stahiki na nafasi yake itatangazwa kwa ajili ya kufanya uchaguzi wa kumchagua mtu atakaeshika nafasi hiyo.
"Nimemsimamisha kazi kupisha uchunguzi hivyo katika kipindi hiki Majukumu yake yatakuwa chini ya Mwenyekiti wa kitongoji cha Mjimwema, na uchunguzi ukikamilika majibu yataletwa kwenye mkutano huu" alisema Mhe Sebabili.
Ameendelea kuwa katika kipindi hiki ambacho Mwenyekiti wa kijiji atakuwa amepumzishwa shughuli zote za kijiji zitasimamiwa na Mwenyekiti wa Kitongoji cha mji mwema Bi. Scholastica ambaye atatekeleza majukumu yote ya kijiji mpaka pale maamuzi mengine yatakapotolewa.
Muheza Mjini, Bomani
Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA
Simu: 027-2977545
Simu ya Mkononi: 0746525653
Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz
Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.